Error message

Deprecated function: Optional parameter $conditions declared before required parameter $data is implicitly treated as a required parameter in include_once() (line 1442 of /home/fawetanzaniaor/public_html/includes/bootstrap.inc).

Shirika lisilo la kiserikali la Forum for African Women Educationalists Tanzania. (FAWETZ) Lenye matawi yake Tanzania Bara  na Visiwani, limetoa mafunzo yaTUSEME  kwa wanafunzi wa shule ishirini na moja(21) Bara na Visiwani.
Tuseme ni programu inayomwezesha mwanafunzi  wa kike na wa kiume, kujitambua na kuona umuhimu wa kuwa shuleni, ambao utasababisha kongezeka kwa mahudhurio shuleni, kupanda kwa Taaluma  na kupunguza Mimba za utotoni pamoja na utoro.

 Wakitoa mafunzo hayo katika Mkoa wa Shinyanga kwenye wilaya ya Shinyanga vijijini, na Kahama na kisiwa cha  Pemba. Mratibu wa shirika hilo Bi Neema Kitundu, akiambatana na wawezeshaji Anne Balisidya, na Octavian Mgaya,  walizifikia shule ishirini na moja, zilizo katika mradi wa “Safe space”(Mahali Salama) unaofadhiliwa na kuendeshwa na shirika la  maendeleo ya elimu sayansi na utamaduni,(Unesco) Tanzania
Shule zilizonufaika na mafunzo yaTuseme katika wilaya ya Kahama  ni shule ya sekondari Lunguya, Mwalugulu, Buliyanhulu, Mwalimu Nyerere Sekondari, Isaka Sekondari, Nyashimbi Sekondari na Kishimba Sekondari.
Aidha katika wilaya ya Shinyanga vijijini wanafunzi wa shule ya sekondari Pandagichiza, Usanda, Iselamagazi, Mwantini, Lyabukande, Ihugi na Tinde Day waliweza pia kunufaika na elimu  hiyo.

 Baada ya mafunzo hayo wanafunzi waliweka maazimio ya kutokukatisha masomo kwasababu zozotezile na kuhakikisha   watafaulu katika masomo yao. Lakini pia watawapa elimu hiyo wanafunzi wenzao ambao hawakupata nafasi ya kushiriki.
Kwa upande wa Tanzania visiwani, shule saba zilizopo Pemba nazo pia zilipata elimu hiyo. Shule hizo ni pamoja na Shule ya sekondari Mgogoni, Micheweni, Chwakatumbe, Tumbe, Shumbavyamboni, Wingwi na Makangale.

Miongoni mwa changamoto zilizobainiwa kusababisha vikwazo kwa elimu ya wasichana na wavulana  ni pamoja na  wasichana kuozeshwa mapema, kupata ujauzito wakiwa shuleni, kupewa kazi nyingi nyumbani na  umbali mrefu kutoka shuleni.

Kwa upande wa wavulana, changamoto wanazokutana nazo ni kuozeshwa mapema, kuchunga, kujitafutia mahitaji wenyewe, hasa baada ya kufiwa na wazazi wao na  kwenda kuvua.
 
Ikiwa ni sehemu ya mafunzo haya ya TUSEME, yalifanyika maonyesho yaliyowashirikisha  wazazi na walezi wa wanafunzi pamoja na wanafunzi  na walimu wao, yaliyokuwa na lengo la kuibua mikakati  shirikishi ya kuondoa vikwazo hivyo  kwa pamoja yaani wanafunzi,waalimu na jamii inayozunguka shule kuunganisha jitihada ili kuwepo na elimu bora kwa manufaa ya watoto,wazazi na Taifa kwa ujumla.